• Barua pepe |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Mrejesho na Malalamiko |
RORYA DISTRICT COUNCIL
RORYA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA RORYA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Elimu Sekondari
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu na Maendeleo ya Vijjiji na Miji
      • Mipango and Uratibu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA)
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • TASAF
      • Ardhi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
    • Kata
      • Kata za Tarafa ya Nyancha
        • Kata ya Kigunga
        • Kata ya Kinyenche
        • Kata ya Raranya
        • Kata ya Mkoma
        • Kata ya Bukura
        • Kata ya Tai
        • Kata ya Nyahongo
        • Kata ya Kirogo
        • Kata ya Nyamtinga
        • Kata ya Nyamagaro
        • Kata ya Kyangasaga
      • Kata za Tarafa ya Girango
        • Kata ya Mirare
        • Kata ya Kitembe
        • Kata ya Goribe
        • Kata ya Ikoma
        • Kata ya Koryo
        • Kata ya Bukwe
        • Kata ya Roche
      • Kata za Tarafa ya Luoimbo
        • Kata ya Nyathorogo
        • Kata ya Nyaburongo
        • Kata ya Rabour
      • Kata za Tarafa ya Suba
        • Kata ya Kisumwa
        • Kata ya Nyamunga
        • Kata ya Baraki
        • Kata ya Komuge
        • Kata ya Kyang'ombe
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Tarajiwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari

KUPATA LESENI ZA BIASHARA

UTARATIBU WA KUPATA LESENI ZA BIASHARA

Leseni zote za biashara zinazotolewa na halmashauri, yaani Leseni Kundi B kwa sasa hutolewa kupitia Mfumo mpya wa kukusanya Mapato ya Serikali unaojulikana kwa jina la tausi.

Mfumo huo unapatikana kupitia Anwani ya https://tausi.tamisemi.go.tz/

Mfanyabiashara atabofya kiungio au link hapo juu atajisajili na kukamilisha uombaji. Atapata Namba ya Malipo yaani Control Number na akimaliza kufanya Malipo atapata Leseni yake kwenye Mfumo wa TAUSI popote alipo.

Leseni zote za Biashara hutolewa chini ya Sheria ya Biashara Na. 25 ya mwaka 1972 na marekebisho yake yaliyofanyika mwaka 1980. 

Leseni za vileo hutolewa kwa vipindi viwili (2) ambapo kipindi cha kwanza huanzia tarehe 1/04 hadi 30/09 na kipindi cha pili huanzia tarehe 1/10 hadi 31/03 mwaka unaofuata.

Kwa leseni zinazodhibitiwa na Mamlaka mbalimbali, Kwa mfano (TFDA, EWURA, TIRA, CRB, TILLI) n.k lazima mwombaji kuwa na cheti kutoka Mamlaka husika kabla ya kuomba leseni ya biashara. 

MAHITAJI MUHIMU WAKATI WA KUOMBA LESENI KWA NJIA YA MTANDAO

  1. Jina la Biashara kama sio mtu binafsi (Certificate of Incorporation or Registration)
  2. Memorandum and Article of Association” kama ni Kampuni
  3. Kitambulisho cha Taifa, Cheti cha kuzaliwa au Hati ya kiapo kuonyesha kuwa ni Mtanzania na Mgeni Hati ya kuishi nchini daraja la “A” (Residnece Permit Class “A”).
  4. Hati ya kiuwakili (Power of Attorney) kama wenye hisa wote wa Kampuni wapo nje ya nchi.
  5. Ushahidi wa maandishi kuwa una mahali pa, kufanyia biashara (Kwa mfano hati za nyumba, mkataba wa upangishaji, risiti za malipo ya kodi za majengo au ardhi.
  6. Hati ya kujiandikisha kama mlipa kodi TRA (TIN).

Leseni za Biashara zimegawanyika katika makundi mawili:

LESENI KUNDI A: 

Leseni hizi hutolewa na Wizara ya viwanda na Biashara ambazo ni;

  • •Uagizaji wa bidhaa toka nje (Import license)
  • •Kusafirisha bidhaa nje (Export license)
  • •Wakala wa mali (Estate Agent)
  • •Hotel za Kitalii (Tourist Hotel & Lodging)
  • •Wakala wa kupokea na usafirishaji mizigo (Clearing & Forwarding & Freight forwarders) nk.


LESENI KUNDI B: 

Hizi ndio Leseni zinazotolewa na Halmashauri.  

Mifano ya Leseni hizi ni:

  • •Wakala wa Bima (Insurance Agent) 
  • •Vipuri (Spare parts, Machine Tools) 
  • •Maduka ya dawa za binadamu/ Mifugo 
  • •Viwanda vidogo (Small scale manufacture and selling)
  •  •Uuzaji wa bidhaa Jumla na rejareja (Wholesale & Retail trade)
  • Huduma ya bar, nyumba za kulala wageni (guest/lodge)
  • Uuzaji wa Chakula


MASHARTI YA KUOMBA NA KUPEWA LESENI ZA BIASHARA

i.Mfanyabiashara anapaswa awe na hati ya usajili iwapo anatumia jina la biashara (Certificate of Registration or Incorporation)

ii.Kama ni Kampuni mwombaji awe na “Memorandum of Article of Association” ambazo zinaonyesha kuwa kampuni imeruhusiwa kufanya biashara anayoiomba.

iii.Awe na mahali/ Eneo linalokubalika kwa aina ya biashara anayoiomba naisiwe vibanda vilivyopo kando kando ya barabara.

iv.Mfanyabishara aje na kivuli cha Cheti cha namba ya mlipa kodi (TIN) pamoja na kivuli cha cheti kinachoonyesha kuwa umelipa mapato kwa mujibu wa Sheria (Tax Clearance) ambavyo vyote vinatolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

v.Masharti mengine ya kupata Leseni hutegemea aina ya biashara mtu anayetaka kuanzisha eg. Mgahawa inadidi afuate taratibu zote za afya na kupima wafanyakazi wake.

vi.Hati ya Utaalamu (Professional Certifucates) kwa biashara zote za kitaalam.


MALIPO

Serikali ilirudisha rasmi utoaji wa ada za leseni za biashara kupitia Sheria ya Fedha na 5 ya mwaka 2011. Kutokana na marekebisho hayo, Utaratibu wa kutoa leseni za biashara bila malipo uliondolewa na kurudishwa ada ya Leseni kuanzia tarehe 30 Juni, 2013.

Kiwango cha ada ya leseni kinatofautina kulingana na aina ya biashara husika na eneo ilipo biashara hiyo. Mfano: Kiwango cha ada za Lesseni kwa Halamshauri ya Jiji na Manispaa ni tofauti na za Halamshauri ya Wilaya na maeneo ya vijijini.

Baada ya ulipaji wa ada hiyo mfanyabiashara atapatiwa Stakabadhi kwa malipo halali ya Fedha yake.


Adhabu

Mnyabiashara atakayekutwa anafanya biashara bila kuwa na Leseni atatozwa faini ya kuanzia Shs 50,000/= - hadi 300,000/= au apelekwe mahakamani hii imeainishwa kutoka kifungu Na. 10 (1) (b).


WAJIBU WA MFANYABIASHARA

•Kulipia kila mwaka Lesseni ya Biashara yako kwa mujibu wa makadirio

•Ni jukumu la kila mfanyabishara kumiliki lesseni katika eneo lake la biashara na kuiweka mahala pa wazi ili kuonekana kwa urahisi.

Matangazo

  • INTERVIEW RESULTS( MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II) October 10, 2024
  • INTERVIEW RESULTS(DEREVA DARAJA LA II) October 11, 2024
  • RIPOTI KUU YA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA 2022/2023 April 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 24, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • ZOEZI LA KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA WA SERIKALI ZA MITAA

    October 11, 2024
  • Dc Rorya Dkt Haule alitembelea na kukagua ujenzi wa madarasa 2 na ofisi mmoja ya Walimu shule mpya ya sekondari Kirongwe.

    September 19, 2024
  • kukagua ujenzi wa chuo cha VETA Rorya tarehe 26/9/2024.

    September 26, 2024
  • MWENGE OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE

    July 29, 2024
  • Angalia Vyote

Video

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI
Video Zingine

Kiunganishi cha Haraka

  • Organization Structure of Rorya
  • Photo Gallery

Tovuti zenye Uhusiano

  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Tanzania
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA)
  • Tovuti ya Mkoa wa Mara
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania(NECTA)
  • Chaneli ya Ikulu ya Tanzania

Wanaotembelea tovuti Ulimwenguni

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    INGRI JUU - RORYA

    Sanduku la Posta: 250 TARIME

    Simu ya Mezani: 0282985583

    Simu ya Mkononi :

    Barua Pepe za Watumishi: mkurugenzi@roryadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Wanaotembelea Tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Zote Zimehifadhiwa